Wakimbizi wa Burundi hawana matumaini

Wakimbizi wa Burundi hawana matumaini
Wakimbizi wa Burundi waliokimbilia nchini Rwanda kufuatia machafuko ya kisiasa yanayoendelea nchini kwao wamepoteza matumaini ya kumalizika haraka mgogoro wa nchi yao.
Raia hao wa Burundi wapatao elfu 25 ambao wamekuwa wakiishi mjini Kigali huko Rwanda tangu nchi yao ilipotumbukia katika lindi la machafuko, wamesema kuwa, wamekosa matumaini ya kurejea makwao hivi karibuni na kwamba bado wanasubiri utatuzi wa kadhia hiyo.
Kwa mujibu wa wakimbizi hao, magogoro wa sasa nchini Burundi unashabihiana sana na ule wa Rwanda kabla ya kutokea mauaji ya kimbari ya mwaka 1994. Wameongeza kuwa, kukosekana makubaliano baina ya serikali na wapinzani ndiyo sababu kuu iliyowafanya kukosa matumaini ya kuweza kuhitimishwa machafuko nchini Burundi. Wanyarwanda karibu milioni moja waliuawa katika mauaji ya kimbari ya mwaka 1994.
Kwa mujibu wa Umoja wa Mataifa, hadi sasa machafuko nchini Burundi yamesababisha mamia ya watu kuuawa na wengine zaidi ya laki mbili kuwa wakimbizi. Wakimbizi elfu 75 kati yao wamekimbilia nchini Rwanda na elfu 25 miongoni mwao wanaishi mjini Kigali.(VICTOR)

Comments

Popular posts from this blog

Locanda La Scuola, Lusiana / Italy

Adult film star has shocking freak accident with his eggplant (photos)

Director Nisher; Nini Kimepoteza Umaarufu Wa Kazi Zake.