Posts

NEWS:Makonda afunguka kuitwa na Bunge Kujieleza

Image
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda amesema hawezi kufika mbele ya Kamati ya Haki, Kinga na Madaraka ya Bunge kuhojiwa kwa kuwa hajapokea barua ya kuitwa. Makonda jana alisema hatoweza kwenda mbele ya kamati hiyo bila barua rasmi iliyomtaka kufanya hivyo. Bunge lililokuwa likiendelea na vikao vyake Dodoma kabla ya kuahirishwa juzi, lilipitisha uamuzi wa kuwataka Makonda na Mkuu wa Wilaya ya Arumeru, Alaxander Mnyeti, kufika mbele ya kamati hiyo na kuhojiwa kutokana na kauli walizozitoa, zinazodaiwa kuudharau mhimili huo wa dola. Lakini Makonda alisema jana “hilo suala la mimi kuitwa kwenye kamati nalisikia na kulisoma kwenye magazeti." "Sina uhakika ni lini wamefikia uamuzi huu wa kuniita na hata kama wamefikia uamuzi huo, sijaletewa barua rasmi.” Baada ya Bunge kupitisha uamuzi huo wa kuitaka Ofisi ya Bunge iwaandikie barua viongozi hao, juzi baadhi ya wabunge walihoji kauli ya Katibu wa Bunge, Dk. Thomas Kashililah,

BREAKING NEWS: Majina Ya Wanafunzi Waliopata Mkopo Baada Ya Kukata Rufaa Bodi Ya Mikopo 2016/2017

Image
Bodi ya Mikopo imetangaza majina ya wanafunzi waliofanikiwa kupata mkopo baada ya kukata rufaa. ==> << BOFYA HAPA >>  Kuyatazama majina hayo

Basi la Kampuni ya Tahmeed Lateketea Kwa Moto

Image
Basi la Abiria la Kampuni ya TAHMEED linalofanya safari zake kati ya Tanga- Dar es Salaam, limeteketea kwa moto katika barabara ya Chalinze- Segera. Taarifa kutoka eneo la tukio zinaeleza kuwa hakuna mtu aliyefariki wala kujeruhiwa kutokana na ajali hiyo lakini mizigo ya abiri ndiyo imeteteketea ndani ya basi hilo. Ajali imetokea wakati basi hilo likiwa limesimama baada ya Abiria mmoja kuomba Msaada akajisaidie (kuchimba dawa) na ndipo abiria waliokuwamo ndani ya gari alianza kusikia harufu ya moshi wa tairi linaloungua na ndipo wakatoka nje ya gari na muda mfupi gari lote likashika moto.

Diamond Platnumz Afunguka Kuhusu Wema Sepetu

Image
Akiwa kwenye kipindi cha Friday Night Live cha EATV, Diamond Platnuzm amesema kitendo alichofanya Wema kupost kazi zake anadhani imefika wakati labda Wema Sepetu ameona hakuna sababu yeye kuendelea kumchukua Diamond Platnumz na ndiyo maana ameonyesha upendo kwa kusupport kazi zake na za wasanii kutoka kwenye Label yake. “Kuna wakati inafika watu mnakuwa mmekuwa labda, mtu anaona hana sababu ya kuendelea kukuchukia au kuwa na vita na wewe, sababu mwanzo mwanzo mkiwa bado mnaenda mnaona kuna vitu mko navyo ndiyo maana kuna kuwa na chuki kubwa, lakini ikifika wakati kila mtu amesonga mbele na maisha yake, ameridhika na maisha yake anaona kwanini nimuwekee vita mtu fulani hivyo nadhani labda wakati huo ndiyo huu maana mwenyewe nimeona kweli amepost BET, amepost promo ya Rich Mavoko kwangu mimi nafurahi kwa sababu naona haina faida kwa sisi wasanii kuwekeana vita” alisema Diamond Platnumz Mbali na hilo Diamond Platnumz alidai toka ameachana na Wema Sepetu ha

Babu Tale asema ni bahati kwa wasanii wa ‘WCB’ kupata wanawake wenye umri mkubwa zaidi yao (Video)

Image
Baada ya kambi ya WCB kuonekana wasanii wake wanapenda kutoka kimapenzi na wanawake wenye umri mkubwa zaidi yao, uongozi wa kambi hiyo umelizungumzia swala hilo. Diamond, Harmonize Akizungumza na waandishi wa habari Alhamisi hii, Mmoja kati ya viongozi wa juu wa kambi hiyo, Babu Tale, amesema ni bahati kwa wasanii wake kupata wanawake waliowazidi umri. “Sisi tunameneji wasanii hatumeneji hisia zao, lakini ikitokea msanii fulani amempenda mwanamke fulani tunamuacha kwa sababu ni mapenzi yake,” alisema Tale. “Tunaona ni bahati kwa wasanii wetu kupata wanawake waliowazidi umri, hiyo ni bahati (anacheka) kwa sababu wanamuenzi Mtume Muhammad (s.a.w.w.) alimuoa Bi Khadija ambaye alimzidi umri,” Hata hivyo, Tale alisema ndani ya WCB hawameneji mapenzi bali wanammeneji msanii pamoja na kazi zake.

BAADA YA KUTOA MAREKANI MTOTO GETRUDA CLEMENT AKARIBISHWA BUNGENI LEO.

Image
Getrude Clement mwenye umri wa miaka 16 ambaye ni mwanafunzi wa kidato cha tatu anayesoma shule ya Sekondari Mnarani iliyopo jijini Mwanza, leo amepata nafasi ya kufika bungeni Dodoma baada ya kupewa mwaliko wa Serikali  Hivi karibuni Getrude  alihutubia viongozi mbalimbali wa dunia kwenye mkutano wa Umoja wa Mataifa uliohusu mabadiliko ya tabia nchi uliofanyika New York Marekani ambapo leo Bungeni  amewahimiza Watanzania kutunza mazingira na kufuata maelekezo yanayotolewa na Serikali na wataalamu wa mazingira ili kuyatunza mazingira wanamoishi. Getrude amesema kuwa amefarijika kwa kuwawakilisha vijana wa Tanzania na dunia kwenye mkutano wa mabadiliko ya tabia nchi ambapo mataifa 175 yalikutana kusaini makubaliano ya Paris. Katika kuwahimiza vijana kujenga tabia ya kutunza mazingira, Getrude amewaasa vijana hasa wanafunzi kusimamia suala la utunzaji wa mazingira wakiwa shuleni kwa kwa kujiunga na klabu mbalimbali ambapo yeye amejiunga na klabu ya

Kigogo Aweka Majina Hewa Mradi wa Tasaf...Wananchi Wamtusua Jipu...

Image
 WANANCHI wamemkataa mwenyekiti wa kitongoji cha Mwanogi kijiji cha Bulima, Kata ya Nyashimo wilayani hapa katika Mkoa wa Simiyu, wakimtuhumu kuweka majina hewa katika mradi wa kuokoa kaya masikini unaosimamiwa na Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (Tasaf). Mwenyekiti huyo wa kitongoji, Ester Ng’ombe anatuhumiwa pia kufanya kazi kwa ubaguzi wa vyama vya siasa. Akizungumza katika kikao, mwenyekiti wa kamati ya mipango na fedha ya kijiji cha Bulima, Zablon Ntinika alisema wamefikia uamuzi wa kumsimamisha kazi mwenyekiti huyo baada ya uchunguzi walioufanya kubaini majina matano ambayo ni hewa yakipatiwa fedha. Alisema wamekuwa wakifuatilia kwa karibu mwenendo wa mwenyekiti huyo katika utendaji wake wa kazi katika kitongoji hicho lakini wamebaini mengi. Mwenyekiti huyo anayetuhumiwa, alipoulizwa kuhusu madai hayo, alisema kuwa yeye hayatambui bali ni siasa za chuki dhidi yake. Ng’ombe alisema chanzo si majina feki bali ni siasa zinazochochewa na